Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Friday, 27 December 2013

Kuku Kidari Kwa Sosi Ya Malai



Mahitajio
Utayarishaji
Kipimo

Kuku bila ya mfupa (kidari)
katakata osha
1 kilo
Kitunguu maji
katakata (chop)
2
Tungule/nyanya
    “
2
pilipili mbichi/shamba kijani
Saga
3
Kitunguu thomu/saumu
katakata (chop)
7-10 chembe
Tangawizi mbichi
saga
1 kipande
chumvi

kiasi
Pilipili nyekundu ya unga

1 kijiko cha chai
Malai (cream)
tumia ya tayari
1 gilasi
Bizari pilau/ jiyrah/cummin

1 kijiko cha chai
Gilgilani/Dania/corriander

1 kijiko cha chai
Mafuta

1/3 kikombe

Namna Ya Kupika:
  1. Weka mafuta katika sufuria, kaanga vitunguu maji hadi vilainike- Usiache mpaka vikageuka rangi sana.
  2. Tia kitunguu thomu/saumu na tangawizi mbichi endelea kukaanga.
  3. Tia vipande vya kuku, endelea kukaanga kidogo
  4. Tia nyanya, bizari zote, chumvi, pilipili mbichi endelea kukaanga
  5. Mwishowe tia malai , changanya vizuri, acha ichemke kidogo kuku aive.
  6. Ongezea malai mwishoni baada ya kuzima moto, changanya vizuri, epua.

No comments:

Post a Comment