Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Wednesday, 1 January 2014

Tambi Za Nazi


 
 VIPIMO

Tambi za Mchele
Pakti 1 (400 mg)

Tui la nazi
Kikombe 1

Sukari
Nusu kikombe, ukipenda ongeza kidogo

Maziwa ya kopo (evaporated)
Nusu kikombe

Samli
Kijiko 1 cha supu

Zabibu kavu
¼ Kikombe

liki
¼ kijiko cha chai

'Arki (rose flavour)
Matone matatu au zaidi



NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA
  
1)       Chemsha tambi kidogo tu katika maji   yanayochemka   na uzichuje  
          (zisiwive)  
2)      Chemsha tui la nazi, pamoja na vitu vyote vingine, koroga
          vichanganyike  katika moto.
3)      Tia tambi na koroga vizuri.
4)     Karibu na kukauka tui  mimina tambi katika treya ya kupikia na zitie katika jiko (oven) zipike kwa moto wa 350 Deg. mpaka zikauke. (kama dakika 15 )  Kisha zima moto wa chini na washa moto wa juu zigeuge rangi kidogo.
5)     Ziepue na zipakue katika sahani zikiwa tayari kuliwa.

No comments:

Post a Comment