
Vipimo
Unga 2 vikombe
Baking Powder 2 vijiko vya chai
Sukari ½ kikombe
Yai 1
Maziwa 1 ¼ kikombe
Maziwa ya mvuke (evaporated milk) ¾ kikombe
Siagi 1 Kijiko cha supu
Mjazo
Jamu ya Stroberi 1 kijiko cha chai
*Chokoleti kiasi
Sukari ya unga 1 kijiko cha chai
Yayusha baadhi ya chokoleti na kipande kimoja acha kando
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
- Tia unga, baking powder na sukari katika bakuli.
- Weka yai, maziwa yote na siagi katika bakuli jengine na upige kwa wiski (whisk – mwiko wa kupigia mayai) hadi ichanganyike, kisha changanya katika unga na endelea kupiga kwa wiski hadi uchanganyike vizuri na uwe nyororo.
- Weka motoni kikaango kisichoganda (non-stick frying pan), moto baina ya mdogo na wastani.
- Chota kwa mwiko kiasi nusu 1/3 kikombe (au takriban ½ kikombe) mimina katika kikaango.
- Subiri itoe viputo (bubbles) kisha geuza upike upande wa pili. Pande zote ziive kugeuka rangi ya dhahabu.
- Epua weka kando huku ukimaliza kupika mikate mingine.
- Panga katika sahani na fanya sandwich kwa kutia jamu ya stroberi.
- Nyunyizia chokoleti juu yake na weka kipande kimoja cha chokoleti juu yake.
- Nyunyizia sukari ya unga ikiwa tayari
Kidokezo:
Kipimo Cha kiasi mikate 15
No comments:
Post a Comment