
Mahitajio
|
Utayarishaji
|
Kipimo
|
Makaroni
|
500 gms
| |
Kitunguu maji
|
Katakata (chop)
|
1
|
Nyanya/tungule
|
Katakata vipande vidogodogo (dice)
|
3
|
Kitunguu thomu
|
Saga au katakata (chop)
|
1 kijiko cha supu
|
Zuchini
|
kata slesi za round
|
2
|
Pilipili boga (capsicum)
|
katakakata
|
1
|
Chumvi
|
Kisia
| |
Pilipili manga
|
1 kijiko cha chai
| |
Mafuta
|
2 vijiko vya supu
|
Namna Ya Kupika:
- Chemsha makaroni yaive, chuja maji. Tia siagi kidogo yasigandane.
- Katika sufuria, weka mafuta, kaanga vitunguu hadi vilainike na kugeuka rangi kidogo.
- Tia kitunguu thomu kaanga.
- Tia nyanya, pilipili manga, chumvi changanya vizuri.
- Tia slesi za zuchini, na pilipili boga funika kidogo viive kidogo.
- Tia makaroni, changanya vizuri yakiwa tayari kuliwa na sosi ya nyama.
Sosi Ya Nyama:
Mahitajio
|
Utayarishaji
|
Kipimo
|
Nyama ng’ombe
|
Katakata vipande vidogo kiasi
|
½ kilo
|
Tangawizi mbichi
|
saga
|
1 kijiko cha chai
|
Kitunguu thomu
|
saga
|
1 kijiko cha chai
|
Kitunguu
|
Katakata (chop)
|
1
|
Nyanya kopo (paste)
|
3 vijiko vya supu
| |
Kotmiri
|
Katakata (chop)
|
½ kikombe cha chai
|
Oregano (bizari ya pasta)
|
1 kijiko cha chai
|
Namna Ya Kupika:
- Weka nyama katika sufuria, tia tangawizi mbichi, kitunguu thomu, chumvi changanya vizuri.
- Funika uchemshe nyama hadi iwive na kukaribia kukauka.
- Tia mafuta, vitunguu, nyanya, nyanya kopo, oregano, changanya vizuri uendelee kupika.
- Ikiwiva tia kotmiri, zima moto ikiwa tayari kuliwa na makaroni.
No comments:
Post a Comment